Monthly Archives: Oktoba 2014

FBME Yasema Asante kwa ‘Wadau’

Septemba 3, 2014

FBME Limited ilituma ujumbe wa shukrani kwa wale watu mbalimbali na mashirika ambayo wamejitokeza kutoa msaada kwa Benki katika mapambano yake dhidi ya Azimio na hatua zilizowekwa dhidi ya tawi la Cyprus. Kuna uvumi wa wazi ulioenea kwa umma kwamba hatua zilizochukuliwa na Benki Kuu ya Cyprus zimekuwa za haraka sana, si za haki na zenye madhara makubwa. Kuna ukimya wa kimataifa kuhusu matendo ya mamlaka ya benki ya Cyprus dhidi ya tawi la benki ya kigeni, wakati hatua hizo zimechukuliwa bila kushauriana na Mwangalizi Mkuu aliyepo Makao makuu nchini Tanzania.

Malalamiko Yamiminika kwa msimamizi Maalum

Agosti 22, 2014

Kuendelea kuzuia miamala kwenye tawi la Benki ya FBME Cyprus kumeleta malalamiko zaidi ya 1,000 yaliyoandikwa na ya maongezi kwa Msimamizi Maalum wa Benki Kuu ya Cyprus. Kilichoanza kama tone, kikageuka kuwa mafuriko na sasa kimekuwa tsunami. Mapendekezo yametolewa kwamba Msimamizi Maalum huenda alizidisha mamlaka yake chini ya Azimio Maalum tangu kuteuliwa kwake tarehe 21 Julai. Inasemekana pia kuwa amekuwa ni kiini cha kesi iliyoko mahakamani kama inavyosemwa na walalamikaji.

Continue reading