Monthly Archives: Mei 2015

Dhambi: Zile za Mapungufu na Zile za Utendaji

9 Mei 2015

Tarehe 21 Julai, 2014 mnamo saa 5 usiku, Benki Kuu ya Cyprus ilitangaza kuanza kwa hatua ya Azimio kwa tawi la benki ya FBME la Cyprus. Kama tujuavyo, Azimio ni njia inayotumika kwa uendeshaji wa shughuli zote za benki inayofilisika, lakini haijatumika kwa benki iliyo na fedha, yenye ukwasi wa kutosha kama FBME tawi la Cyprus. Katika kuifikia hatua hii, Benki Kuu ilishindwa kuratibu – au hata kuijulisha – Benki Kuu ya Tanzania ambayo ni Msimamizi Mkuu wa Makao Makuu ya Benki ya FBME. Kuanzia siku hiyo hadi sasa, CBC imeshindwa kuunganisha matendo yake na yale ya mamlaka kuu nchini Tanzania au hata kufuata kanuni na sheria za Cyprus na Umoja wa Ulaya (EU).

Continue reading

Wasimamizi Wawili wa FBME Kulipwa zaidi ya Gavana wa CBC na Mario Draghi – Kwa Pamoja

Mei 5, 2015

Ukweli wa mambo umeibuka kutokana na maelezo ya uteuzi wa msimamizi wa pili wa Benki Kuu ya Cyprus (CBC) kuendesha tawi la Benki ya FBME la Cyprus. Wasimamizi hawa wawili wanalipwa zaidi ya mishahara (kwa pamoja) ya Gavana wa CBC na mtu anayemtambua kama bosi wake, Rais wa Benki Kuu ya Ulaya – ECB, Mario Draghi. Pengine unaweza pia kuunganisha mishahara ya wafanyakazi wengine wa Bodi ya Wakurugenzi ya CBC na bado ukabaki na chenji.

Continue reading

Wafanyakazi Hawahusiki

3 May 2015

Taarifa za hivi karibuni zilieleza kimakosa kuwa wafanyakazi wa FBME wamekwenda Polisi na Benki Kuu ya Cyprus kupeleka madai yasioeleweka kuhusiana na ukiukwaji wa mfumo wa kupambana na pesa chafu. Ukweli ambao FBME inauelewa ni kwamba, watu wanaozungumziwa ni watu binafsi wanaohusishwa na makampuni ya Uingereza ambayo kwa sasa wako katika madai na FBME kuhusu mgogoro wa ankara zilizokataliwa na huduma.

Continue reading