Monthly Archives: Aprili 2016

Profesa wa Marekani: “Kujiamini kwa Kupitiliza” kwa FinCEN Kunahitaji Usimamizi”

Aprili 16, 2016

 

Akiandika kwenye tovuti ya Amerika Banker, Sharyn O’Halloran, Profesa wa George Blumenthal wa Uchumi Siasa na Profesa wa masuala ya kimataifa na ya umma katika Chuo Kikuu cha Columbia, aliandika kwamba katika vitendo vyake dhidi ya FBME ni wazi kwamba “… Kujiamini kupita kiasi kwa FinCEN kunahitaji uangalizi zaidi” kutoka mamlaka za Marekani. Aliyaelezea mapendekezo ya adhabu ya FinCEN kama ya “kibabe”, na kuonyesha “… mapengo ya dhahiri katika mchakato wake wa utawala na ukosefu wa vielelezo muhimu katika kutekeleza azma yake kwa FBME, (ambayo) inaonyesha kwamba FinCEN ‘walitembea wakiwa wamelala’ kuelekea kwenye maamuzi yaliyopangwa ya kutaka tu taasisi ifungwe “.

Aliongeza kuwa “… inaonyesha pia kwamba kwa FinCEN kuilenga mipaka ya benki ni kinyume cha katiba,” na anaamini kwamba kwa kupinga mashambulizi ya FinCEN, FBME “… ina kesi nzuri”. Makala kamili inapatikana hapa: http://www.americanbanker.com/bankthink/overzealous-fincen-needs-more-oversight-1080438-1.html

Mwanasheria Mkuu wa Zamani wa Cyprus Aishukia Benki Kuu

Aprili 12, 2016

 Mr Alekos Markides, aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ambaye sasa ni mshauri wa sheria kwenye Benki ya FBME alifanya mazungumzo kwenye vyombo viwili tofauti vya habari; redio ya taifa CyBC (tar 12 Aprili) na MEGA Television (tar 9 Aprili) katika kukabiliana na uanzishwaji wa hivi karibuni wa Mfuko wa Ulinzi wa Amana. Alidai kuwa Benki Kuu imekosa mkakati na sasa inajaribu kukwepesha mustakabali mzima kutokana na jinsi walivyolishughulikia suala hili.

Continue reading

Uanzishaji wa Mfuko wa Ulinzi wa Amana inailinda CBC, sio Wateja

Aprili 10, 2016

 Kufuatia mfululizo wa vitendo viovu, vilivyo kinyume cha sheria, holela na kukosekana kwa uwajibikaji kwa Benki Kuu ya Cyprus ( “CBC”), na kutangazwa kulikocheleweshwa kwa kuanzishwa mfuko wa ulinzi wa amana Aprili 9, 2016 ni hoja ionayokaribishwa, lakini ni miezi 21 baada ya Mamlaka ya Azimio na CBC kuitekeleza dhidi ya Benki ya FBME ( “FBME”).

Continue reading

Uamuzi wa CBC ni Kinyume cha Sheria na Usiofaa

6 Aprili 2016

Msimamizi Maalum wa Benki ya FBME tawi la Cyprus ametoa barua za kuwaachisha kazi wafanyakazi 136 ili kupunguza gharama na kulinda amana. Sababu alizotoa eti ni kubana matumizi na kulinda amana za wateja?! Hivi sasa Benki ina mtaji na akiba ya dola milioni 162 zaidi ya fedha zinazohitajika kufidia amana zote na gharama yoyote itakatwa kutoka kwenye fedha hizi. Pamoja na hayo, sababu inayosemekana kubana matumizi haina maana yoyote kwa wateja. Hakika, kinyume chake, uwezo wa benki wa kuhifadhi mali zake umeathiriwa vibaya kwa sababu ya kuwapoteza wafanyakazi hawa.

Continue reading