Monthly Archives: Novemba 2015

FinCEN Yatakiwa Kukamilisha Mchakato Mpya wa Kiutendaji

Novemba 8, 2015

Pongezi kwa mfumo wa kimahakama wa Marekani, FinCEN imesitishwa kutekeleza maamuzi yake ya kuiwekea vikwazo Benki ya FBME vilivyotishia kuibomoa kabisa ingawaje FBME imekuwa ikishughulikia masuala yote yaliyoibuliwa na mamlaka husika au wakaguzi. Bila maamuzi ya Jaji Cooper, FinCEN ingeweza kuifuta Benki kabisa kutokana na ushahidi ambao FinCEN walisisitiza kuwa ni siri, licha ya ukweli kwamba hakukuwa na msingi halali kisheria wa kuuzuia ushahidi huo.

Continue reading

Hatua Haramu na ya Kukatisha Tamaa ya Benki Kuu ya Cyprus

Novemba 6, 2015

Vyanzo vya habari vinavyopinga hatua zilizochukuliwa na kundi dogo la maafisa wa Benki Kuu ya Cyprus (CBC) dhidi ya Benki ya FBME, vimetahadharisha kwamba CBC inapanga kufilisi tawi la FBME la Cyprus kufuatia taarifa ya FBME kuhusu uamuzi wake wa kuhamisha baadhi ya akaunti za wateja wake kutoka tawi lake la Cyprus kwenda makao Makuu – Tanzania. Lengo likiwa kujinasua kwenye mtego wao wenyewe. Kama ikitekelezwa, hatua hii ya hatari na haramu itapingwa vikali kwa kutumia vifungu mahsusi vya kisheria.

Continue reading

FBME Yaja na Mpango Wa Kuwafungulia Milango Wateja Wake

Oktoba 31, 2015

 Benki ya FBME imeanzisha mipango ya kuhamisha amana zilizoko katika tawi la Cyprus kwenda kwenye ofisi za makao Makuu nchini Tanzania, ambapo kwa njia hii itawawezesha wateja wake kupata fedha zao. Hii inafuatia hali ambapo wateja wamekuwa na vikwazo vya kuchukua kiasi kidogo cha EUR 1,000 kwa wiki na wakati mwingine wamekuwa wakiwekewa Ukomo kwenye akaunti zao kwa amri ya Benki Kuu ya Cyprus (CBC), ambayo walichukua udhibiti wa FBME tawi la Cyprus mwezi Julai 2014.

Continue reading