Msimamizi Arudi

Desemba 15, 2014

Msimamizi wa Benki Kuu ya Cyprus, mwenye wajibu wa kuendesha Benki ya FBME tawi la Cyprus, amerejea leo baada ya kukosekana kusikoelezeka. Kama inavyojulikana, aliondoka saa 7 mchana siku ya Jumanne, na hivyo kuzuia muamala wowote kufanyika kwa wiki nzima. Matokeo haya ni kutokana na hatua ya kibabe inayomwezesha kuidhinisha miamala yote na kukataa kwake kuteua naibu kufanya kazi kwa niaba yake.

Hata hivyo, amesharudi na miamala ya kiwango cha EUR 2,000 kwa siku kwa kutumia hundi – uamuzi mwingine  wa kibabe – imeanza.