CBC Yateua Msimamizi Maalum Mpya

Januari 19, 2016

FBME imearifiwa kwamba Benki Kuu ya Cyprus (CBC) amemteua Msimamizi Maalum mpya kwa tawi la FBME Cyprus. Aliyeteuliwa Januari 11, 2016, akiwa msimamizi wa tatu tangu sakata hili lilipoanza Julai 2014, ni Bwana Chris Iacovides.

Mr Iacovides aliweka wazi jukumu lake kwenye mkutano na viongozi wa Benki ya FBME tawi la Cyprus, ambapo alisema anaiona kazi yake kuwa ni kudumisha na kuhifadhi shughuli za tawi, na kuongeza kuwa hana nia ya kulifungwa au madhara uharibifu zaidi.

FBME haijaona chochote  kilicho rasmi kutoka CBC kwa kumleta Bw Iacovides na haiwezi kutoa maoni kwa wakati huu juu ya mamlaka yake. Tutashuhudia wakati utakapofika, lakini maelezo ya msimamizi mpya yanaonyesha mwanzo mzuri na uteuzi wake unakaribishwa baada ya wiki mbili za mapumziko  tangu kuondoka kwa mtangulizi wake, mwenye makao yake mjini London, Andrew Andronikou.

Uteuzi wa Bwana Andronikou haukuongezewa muda na CBC ulipofika  mwisho tarehe 31 Desemba 2015. Haijulikani kwa nini hili limetokea, lakini ikumbukwe kwamba alikuwa akilipwa kiasi kikubwa cha fedha kwa mwezi cha EUR 50,000 kwa kile alichokiona kama kazi ya muda, ambapo alipata nafasi ya kufanya kazi zake nyingine nchini Uingereza, kama vile utawala wa mgahawa wa Furqani London.

Kwa upande mwingine, Bw Andronikou alishika nafasi ya usimamizi Mei 2015, kufuatia kujiuzulu ghafla kwa Dinos Christofides, Msimamizi wa kwanza, ambaye kwake, lawama nyingi kwa CBC za uendeshaji mbovu wa tawi la FBME ulianzia akisaidiwa na wenzake wa zamani walioko Benki Kuu.