Wafanyakazi wa FBME Wachangia Familia

8 Januari, 2015

Wafanyakazi wa Benki ya FBME na Kitengo cha Kadi cha FBME kwa mwezi Disemba wamejitolea michango ya chakula na vitu vingine kwa familia zenye uhitaji kwenye mpango wa kila mwaka wa kusaidia familia. Mbali na chakula, wafanyakazi hao wamekusanya nguo, mashuka na vitu vingine vya majumbani, wakati wengine wametoa fedha taslimu zilizotumika kununulia vitu mbalimbali. Familia zenye uhitaji zinatambuliwa na mpango huu maalum. Wafanyakazi wa Benki ya FBME na wa Kitengo cha Kadi wamekuwa wakijitolea kwenye mpango huu wa kusaidia familia zenye uhitaji kwa miaka mitatu mfululizo kama sehemu ya mpango mkubwa wa Ujirani Mwema unaofanywa kwa niaba ya Benki.