Author Archives: Editor1

Hatua Zinaendelea Kupata Ukwasi wa Ziada

Novemba 20, 2014

Kwa kufanya kazi kwa ushirikiano wa karibu na Meneja Msimamizi wa Benki Kuu ya Tanzania na Benki ya FBME Dar Es Salaam, FBME Limited inachukua hatua za kupata ukwasi wa ziada kwenye tawi la FBME Cyprus. Hii inafanywa ili kuhakikisha uwepo wa amana ya kutosha kwa wateja kuepuka tatizo la kiwango cha siku cha muamala kilichowekwa na msimamizi aliyeteuliwa na Benki Kuu ya Cyprus.

Continue reading

FBME Yatoa Onyo la Hatua za Kisheria Hapo Baadae

Novemba 12, 2014

Wanahisa wa FBME Limited wameweka wazi kwamba wanaiwajibisha Benki Kuu ya Cyprus na watu kadhaa ndani ya Benki Kuu hiyo kwa uharibifu na hasara iliyoisababishia Benki ya FBME, wateja wake na wamiliki. Watu wanaodhaniwa kuwajibika ni pamoja na Msimamizi Maalum aliyeteuliwa na Benki Kuu ya Cyprus kudhibiti uendeshaji wa tawi la FBME Cyprus.

Continue reading

Masikitiko kwa Mheshimiwa Christofides

Novemba 12, 2014

Bahati mbaya kwa Mheshimiwa Christofides kwa kukosa safari ya kusisimua ya uzinduzi wa benki mpya nchini Cyprus na kwamba mwajiri wake wa zamani, Ancoria Holdings, amepewa leseni ya Benki na Benki Kuu. Itakumbukwa kwamba alijiuzuru kutoka Ancoria siku ya mwisho ya Julai 2014 kwa barua ya kujiuzulu iliyorudishwa nyuma hadi tarehe 28 Julai. Tunadhani hii ilitokea kwa sababu alitambua uwepo wa mgongano wa maslahi kati ya jukumu lake kama Msimamizi wa FBME tawi la Cyprus aliyeteuliwa tarehe 22 Julai na nafasi yake kama ‘kiongozi wa mradi’ kwa Ancoria katika juhudi zake za kupata leseni ya benki.

Mbili kwenye Mstari!

Novemba 7, 2014

Utasifiwa Unapostahili Sifa: Benki Kuu ya Cyprus imekiongezea muda wa leseni Kitengo Cha kadi cha benki ya FBME na hivyo kukipa nafasi ya kuanza biashara tena hapo baadaye. Kwa hiyo, shukrani zetu ziende kwa Benki Kuu, ambayo alijibu maombi ya Kitengo Cha Huduma za Kadi kuendelea na biashara. Kampuni bado imeendelea kusimamishwa, lakini kama leseni bado inaendelea, kuna nafasi ya kuanza tena biashara mara moja vikwazo vitakapoondolewa.

Ni muhimu kukumbuka kwamba hii inafanywa kwa faida ya soko na kwa ajili ya sifa ya mamlaka.

Kamusi ya maneno

Novemba 7, 2014

Kamusi ya maneno yanayotumika katika tovuti hii imeandaliwa ili kuwasaidia wasomaji kufuatilia maendeleo katika suala la Benki ya FBME:

Azimio la Amri: Sheria ya Mikopo na Mashirika Menine ya Cyprus ya 2013. Madhumuni ya Amri hii ni kuboresha mtaji wa benki zisizo na mtaji.

Continue reading

Maswali yasiojibika

Septemba 10, 2014

Benki Kuu ya Cyprus (CBC) bado kujibu maswali kadhaa muhimu kufuatia uamuzi wake wa kutoza Azimio Amri dhidi ya FBME Bank tarehe 21 Julai. Hapa ni yetu Top Ten:

1. Kwa nini CBC kuamua tarehe 21 Julai kuchukua na kujaribu kuuza Cyprus tawi la FBME Bank, nini maendeleo yamepatikana na uuzaji kwamba na kwa nini wamiliki halisi si angalau ushauri?

Continue reading

Maswali yaumizayo yanayojirudia rudia

Oktoba 31, 2014

Vita ya kisheria katika medani ya kimataifa inaendelea baina ya wamiliki wa FBME Bank dhidi ya Benki kuu ya Cyprus kuhusiana na uamuzi wake batili wa uuzaji wa FBME- tawi la Cyprus. Yaliyojiri hivi karibuni ni kukamilika kwa ufunguaji wa kesi iliofanywa na wanahisa wa FBME, katika Mahakama ya Kimataifa ya Biashara, Paris. Benki Kuu sasa inatakiwa kutoa hoja za msingi juu ya vitendo vyake batili na vyenye uonevu kwenye Mahakama hiyo.

 

Continue reading

Mchawi – Bado anatafutwa

Oktoba 30, 2014

Kuna imani miongoni mwa baadhi ya watu kwamba iwapo utauliza swali mara kwa mara itafika hatua kuwa utapata jibu unalotaka. Ni jambo linaloeleweka kuwa mtoto akitaka kitu, mara kwa mara atauliza “Je naweza? Je naweza? Naweza? Yote hayo huyasema kwa  matumaini kwamba mzazi hatimaye ataridhia. Hili hatulitarajii kutoka kwa viongozi waandamizi wa serikali kufanya hivyo, eti?

Continue reading