Author Archives: Editor1

Barua kwa Rais – Wito wa Kuanzishwa Upya Uchunguzi wa Maafisa wa CBC

Desemba 28, 2015

 Mwenyekiti wa Benki ya FBME, Bwana Ayoub-Farid M Saab, ameandika Barua ya wazi kwa Rais wa Jamhuri ya Cyprus, Nicos Anatasiades, kuonyesha madhara makubwa yaliyosababishwa na Benki Kuu ya Cyprus (CBC). Vitendo vya karibuni vya CBC ni pamoja na jaribio la kuifutia leseni, si tu kwa tawi la FBME Cyprus, bali kwa Tanzania pia.

Continue reading

Wenye Hatia Ni Nani?

Desemba 24, 2015

 Tangia Julai 2014, mwanzo wa sakata lake dhidi ya Benki ya FBME, Benki Kuu ya Cyprus (CBC) imewapeleka wadau kwenye mlolongo wa kushangaza wa vitendo visivyo na mantiki vilivyoibua maswali muhimu kuhusu uaminifu wake kama chombo cha serikali katika siasa za kisasa za Ulaya. Kwa kipindi kirefu cha miezi hii 17, CBC ilikuwa kimya kueleza nia yake, na ni hivi karibuni tu ndio wameanza kuonyesha ukweli wa yale yaliokuwa yakiendelea nyuma ya pazia, na hii ni dalili ya kushindwa kwenye vita vya kisheria kwenye midani ya kimataifa.

Continue reading

FBME Yapambana na CBC Kisheria dhidi ya Ubatilishaji wa Leseni Yake

21 Desemba 2015

FBME Limited imetangaza kuwa hatua za haraka za kisheria zitachukuliwa kupinga kusitishwa kwa leseni, kulikofanywa na Benki Kuu ya Cyprus (CBC) dhidi ya Benki ya FBME Tawi la Cyprus, na uamuzi huu kwenye mahakama ya Cyprus.

Tamko la ubatilishaji huo lenye kurasa 9 limewasilishwa leo Desemba 21, 2015, ikilaumu watendaji wengine kwa vitendo vilivyosababishwa na hatua zilizochukuliwa na Bodi ya CBC katika kipindi cha miezi 17, ambayo imetokana na CBC ilipofanya jaribio la uuzaji wa Benki ya FBME ya tawi Cyprus. FBME inapinga kabisa kubatilishwa kwa leseni hiyo.

Hatua hii ya kidhalimu ya CBC dhidi ya FBME, ambayo ni ya hivi karibuni, imesababisha kesi mbili nchini Cyprus na nje ya nchi, na kuziacha mamlaka za Cypruskwenye mlolongo wa madai ya uharibifu mkubwa na fidia.

Barua ya Wazi ya Alekos Markides kwa Rais

Desemba 15, 2015

Mwanasheria Mkuu wa zamani wa Jamhuri ya Cyprus, Alekos Markides ameandika barua ya wazi kwa Rais Nicos Anastasiades, akimuonya madhara kwa jinsi kesi ya Benki ya FBME inavyoshughulikiwa, pamoja na hatua kadhaa za kidhalimu zilizochukuliwa na Benki Kuu ya kisiwa cha Cyprus dhidi ya Benki. Matokeo ya hatua hizi yameivua nguo serikali ya Cyprus na walipa kodi wake kutokana na madai makubwa ya kuichafua hadhi ya Benki.

Kuona tafsiri ya barua ambayo Mheshimiwa Markides ameituma kwa niaba ya wamiliki wa Benki ya FBME, bofya hapa

FinCEN Yatakiwa Kukamilisha Mchakato Mpya wa Kiutendaji

Novemba 8, 2015

Pongezi kwa mfumo wa kimahakama wa Marekani, FinCEN imesitishwa kutekeleza maamuzi yake ya kuiwekea vikwazo Benki ya FBME vilivyotishia kuibomoa kabisa ingawaje FBME imekuwa ikishughulikia masuala yote yaliyoibuliwa na mamlaka husika au wakaguzi. Bila maamuzi ya Jaji Cooper, FinCEN ingeweza kuifuta Benki kabisa kutokana na ushahidi ambao FinCEN walisisitiza kuwa ni siri, licha ya ukweli kwamba hakukuwa na msingi halali kisheria wa kuuzuia ushahidi huo.

Continue reading

Hatua Haramu na ya Kukatisha Tamaa ya Benki Kuu ya Cyprus

Novemba 6, 2015

Vyanzo vya habari vinavyopinga hatua zilizochukuliwa na kundi dogo la maafisa wa Benki Kuu ya Cyprus (CBC) dhidi ya Benki ya FBME, vimetahadharisha kwamba CBC inapanga kufilisi tawi la FBME la Cyprus kufuatia taarifa ya FBME kuhusu uamuzi wake wa kuhamisha baadhi ya akaunti za wateja wake kutoka tawi lake la Cyprus kwenda makao Makuu – Tanzania. Lengo likiwa kujinasua kwenye mtego wao wenyewe. Kama ikitekelezwa, hatua hii ya hatari na haramu itapingwa vikali kwa kutumia vifungu mahsusi vya kisheria.

Continue reading

FBME Yaja na Mpango Wa Kuwafungulia Milango Wateja Wake

Oktoba 31, 2015

 Benki ya FBME imeanzisha mipango ya kuhamisha amana zilizoko katika tawi la Cyprus kwenda kwenye ofisi za makao Makuu nchini Tanzania, ambapo kwa njia hii itawawezesha wateja wake kupata fedha zao. Hii inafuatia hali ambapo wateja wamekuwa na vikwazo vya kuchukua kiasi kidogo cha EUR 1,000 kwa wiki na wakati mwingine wamekuwa wakiwekewa Ukomo kwenye akaunti zao kwa amri ya Benki Kuu ya Cyprus (CBC), ambayo walichukua udhibiti wa FBME tawi la Cyprus mwezi Julai 2014.

Continue reading

Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi ICC inaona inayo mamlaka Kusuluhisha Kesi kati ya Wamiliki wa Benki ya FBME na Jamhuri ya Cyprus

Septemba 16, 2015

 Kwenye maamuzi yake yaliyosainiwa tarehe 10 Septemba 2015, Mahakama ya Kimataifa ya Biashara (ICC) mjini Paris aliamua kwamba ina mamlaka juu ya madai ya wamiliki wa FBME Limited (Wadai) dhidi ya Jamhuri ya Cyprus (Washtakiwa) kuhusu Mkataba wa Lebanon-Cyprus unaosimamia ulinzi wa haki za mwekezaji.

Continue reading